Uncategorized

SIMBA: MCHEZO UTAKUWA MGUMU ILA TUPO TAYARI

admin December 21, 2020 12:47 pm


 UONGOZI wa Simba umesema kuwa upo tayari kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya FC Platinum ambao unatarajiwa kuchezwa Desemba 23, Uwanja taifa wa Zimbabwe.


Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote mbili kutokana na umuhimu wake huku Simba ikiweka wazi kwamba imejipanga kupata matokeo chanya. 


Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez amesema kuwa maandalizi ambayo wameyafanya yanawapa matumaini ya kuweza kupata matokeo ambayo wanayafikiria.

“Kikosi kipo imara na maandalizi yanakwenda vizuri huku na tunaamini kwamba kwa namna ambavyo tumejipanga tuna nafasi ya kupata matokeo.

“Kikubwa mashabiki wazidi kutuombea na kutupa sapoti ili tuweze kushinda mchezo wetu, benchi la ufundi linatambua kwamba mchezo utakuwa mgumu na wenye ushindani ila tupo tayari,” .

Mchezo huo utachezwa majira ya saa 9:00 kwa saa za Zimbabwe ambapo kwa Bongo itakuwa saa 10:00 jioni. 

WANA KINO BOYS KAMILI GADO KUIVAA JKT TANZANIA AZAM: TUNA OFA NYINGI ZA WACHEZAJI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply