Home Uncategorized KIUNGO MSHAMBULIAJI WA SIMBA ALIYEWEKWA KWENYE RADA ZA NAMUNGO ANATIMIZA MIAKA KADHAA

KIUNGO MSHAMBULIAJI WA SIMBA ALIYEWEKWA KWENYE RADA ZA NAMUNGO ANATIMIZA MIAKA KADHAA

0

 


KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Miraji Athuman ambaye anatajwa kuwekwa kwenye rada za mabosi wa Namungo leo Desemba 27 anatimiza miaka 27 ya kuletwa duniani.


Msimu huu wa 2020/21 mambo yamekuwa magumu kwake kupata namba kikosi cha kwanza tofauti na msimu uliopita ambapo alikuwa na nafasi kikosi cha kwanza.


2019/20 alitupia mabao 7 na kutoa pasi moja ya bao majeraha ya mara kwa mara ni moja ya sababu iliyomtoa kwenye reli. Kwa msimu huu wa 2020/21 hajafanikiwa kutupia ndani ya Ligi Kuu Bara.


Huenda mipango ya Namungo ikijibu ya kumuhitaji nyota huyo kwa mkopo anaweza kuendeleza makali yake kwenye kikosi hicho kinachonolewa na Hemed Morroco.