Home Uncategorized YANGA YAIVUTIA KASI NAMUNGO

YANGA YAIVUTIA KASI NAMUNGO

0

 


CEDRIC Kaze, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa kesho wa Kombe la Mapinduzi dhidi ya Namungo FC. 


Yanga ilifungua pazia Januari 6 kwa kucheza na Klabu ya Jamhuri ambapo dakika 90 zilikamilika kwa timu zote kutoshana nguvu.


Mchezo huo ulichezwa saa 8:15 usiku hivyo kesho itakuwa na kazi ya kusaka ushindi mbele ya Klabu ya Namungo.


Kaze amesema:”mchezo wa Kwanza tulikutana na timu nzuri ambayo ilikuwa inapambana ndani ya uwanja tutaingia kwenye mchezo wa pili kwa tahadhari tukisaka ushindi,” .


Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Amaan, saa 8:15 usiku, bingwa mtetezi wa taji hilo ni Mtibwa Sugar ambaye alitwaa msimu wa 2020 kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba.