Yanga SC

BALAMA MAPINDUZI AREJEA NCHINI KUTOKEA SAUZ

admin January 21, 2021 5:47 pm

 KIUNGO mshambuliaji wa klabu ya Yanga, Balama Mapinduzi amerea nchini leo akitokea nchini Afrika Kusini alipokwenda kwa ajili ya matibabu.

Akiwa Afrika Kusini, Balama alifanyiwa upasuaji wa enka na kutokana na upasuaji huo anatarajiwa kuwa nje kwa kipindi cha wiki tano.

Akizungumzia kuhusu matibabu ya mchezaji huyo Ofisa habari wa klabu ya Yanga, Hassani Bumbuli amesema: Balama Mapinduzi amerejea leo kutokea nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kufanyiwa upasuaji, tunatarajia atakuwa nje kwa wiki tano na baada ya hapo tutatoa taarifa zaidi,”

Naye Balama amesema: “Nawashukuru wote ambao wamenisaidia kukamilisha matibabu yangu, naomba mzidi kuniombea ili Mungu akipenda basi nirejee uwanjani,”

HIKI HAPA KIKOSI CHA USAJILI BORA LIGI KUU BARA MSIMAMO WA LIGI KUU YA WANAWAKE TANZANIA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply