Home Azam FC DUBE: KWA BEKI HUYU, SIMBA WAMEPATA JEMBE

DUBE: KWA BEKI HUYU, SIMBA WAMEPATA JEMBE


MSHAMBULIAJI hatari wa kikosi cha klabu ya Azam, Prince Dube amefungukia usajili wa beki mpya wa Simba raia wa Zimbabwe, Peter Muduhwa kwa kusema ni mchezaji mzuri na anaamini kwa kiwango chake Simba hawatajutia kumsajili. 

Muduhwa amekamilisha usajili wa kujiunga na Simba akitokea kikosi cha Highlanders FC ya Zimbabwe ambapo amewahi kucheza na Prince Dube.

Muduhwa alikuwa sehemu ya kikosi cha Zimbabwe kilichokuwa kikishiriki michuano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN).

Muduhwa amekuwa mchezaji wa tano kusajiliwa na Simba katika kipindi cha dirisha dogo baada ya Taddeo Lwanga, Doxa Gikanji, Tatenda Chikwende na Junior Lukosa ambapo timu hiyo inaonekana kujiimarisha kwa ajili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na kombe la Ligi Kuu Bara.

Akimzungumzia beki huyo Dube alisema: “Kwangu ni jambo la furaha kuona ndugu yangu mwingine akija Tanzania, nampongeza kaka yangu Muduhwa kwa kukamilisha usajili wake Simba.

“Ni mchezaji mpambanaji na wa kiwango cha juu, naamini atakuwa msaada mkubwa kwao na namtakia kila la kheri kwenye majukumu yake mapya,”

SOMA NA HII  NDUGU WA SAKHO WA SIMBA AFUNGA USAJILI AZAM....NI 'KITASA CHA KAZI CHAFU HASWA'...YUPO TIMU YA TAIFA YA SENEGAL..