IMEELEZWA kuwa baada ya mabosi wa Simba kushindwana na Florent Ibenge ambaye ni Kocha Mkuu wa AS Vita pamoja na timu ya Taifa ya Congo kwenye upande wa maslahi sasa wameelekeza nguvu kwa Didier Gomes Da Rosa.
Ibenge alikuwa anatajwa kuwa kwenye rada za Simba kuja kuchukua mikoba ya Sven Vandenbroeck ambaye alibwaga manyanga Januari 7.
Didier anatajwa kujiunga na Simba akitokea katika Klabu ya EL Marreikh ya nchini Sudan ambapo inasemekana kuwa amevunja mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo.
Hizi hapa timu alizowahi kuzifundisha, 2008–2010 AS Roquebrune Cap Martin, 2010–2010 ES Fos sur Mer
2010–2011 Cagnes-le-Cros, 2012–2013 AS Cannes B
2013–2014 Rayon Sports, 2014–2015 Coton Sport, 2015–2016 CS Constantine, 2016–2017 JSM Skikda, 2017–2018 Ethiopian Coffee, 2019 Horoya AC, 2019–2020 Ismaily na 2020- Al-Merrikh.