KIKOSI cha Namungo FC kimewasili leo Januari 6,2020 salama kwenye ardhi Dar es Salaam kikitoka Sudan.
Jana Januari 5 kilikuwa na mchezo wa Kombe la Shirikisho wa marudio dhidi ya Al Hilal Obeid ambapo ililazimisha sare ya kufungana mabao 3-3.
Sare hiyo inaifanya timu hiyo iwaondoshe wapinzani hao kwa jumla ya mabao 5-3.
Mchezo wa kwanza waliocheza Uwanja wa Azam Complex, Namungo FC ilishinda mabao 2-0.