Home Yanga SC YANGA WAREJESHA KWA JAMII,GHANA NA BONGO

YANGA WAREJESHA KWA JAMII,GHANA NA BONGO

 


MICHAEL Sarpong mshambuliaji ndani ya kikosi cha Yanga alipata nafasi ya kutoa msaada kwenye kituo cha Royal Seed Orphanage kilichopo nchini Ghana wiki hii.

Sarpong alirejea Ghana, Januari 13 baada ya kumaliza kazi ya kusaka Kombe la Mapinduzi Visiwani Zanzibar.

Ndani ya Ligi Kuu Bara ametupia mabao manne wakati timu yake ikiwa nafasi ya kwanza kwenye msimamo na anatarajiwa kurejea leo kujiunga na kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu, Cedric Kaze.

Pia nyota mwingine ambaye alifanya kama Sarpong kwa kurejesha kwa jamii ni Mukoko Tonombe ambaye yeye jana Januari 24 alitembelea kituo cha watoto yatima cha Maunga Centre kilichopo Kinondoni, Mkwajuni.

SOMA NA HII  BAADA YA KUIZOEA TIMU MPYA...NKANE AFICHUA SIRI ZA YANGA HADHARANI...AANIKA HOFU ALIYONAYO...