KLABU ya Yanga leo Aprili 21 imeingia kwenye mkataba wa makubaliano ya ushirikiano na Klabu ya Raja Club Athletic ya nchini Morocco.
Ushirikiano huu ambao wameingia Yanga utahusisha masuala mbalimbali ya maendeleo baina ya klabu hizi mbili zenye historia kubwa Barani Afrika.
Klabu ya Raja kwa sasa ipo ardhi ya Bongo ambapo leo ilikuwa na kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Namungo FC, Uwanja wa Mkapa.
Ikiwa ipo hatua ya makundi imeshinda kwa mabao 3-0 dhidi ya Namungo na kusepa na pointi tatu mazima.