Home kimataifa BARCELONA YAMALIZANA NA MAJEMBE MANNE

BARCELONA YAMALIZANA NA MAJEMBE MANNE


 TIMU ya Barcelona imezidi kujiimarisha baada ya kukamilisha dili la miaka miwili kwa mshambuliaji Memphis Depay kutoka Lyon.

Timu hiyo ilikuwa inaipigia hesabu saini ya nyota huyo kwa muda mrefu na mwisho wa siku walifanikiwa kumpata mchezaji huyo na kumpa dili la miaka miwili ataondoka hapo mwaka 2023 ikiwa mabosi hao hawatakuwa tayari kumpa dili jipya.

Staa huyo alijenga jina lake akiwa ndani ya Manchester United kabla hajatua Lyon hivi karibuni aligoma kusaini dili jipya na timu hiyo ya Ufaransa.

Anakuwa ni mchezaji wa nne Barcelona inayonolewa na Kocha Mkuu, Ronald Koeman kusajiliwa kwenye usajili huu baada ya kuanza na Sergio Arguero, Eric Garcia na Emerson Royal.  


SOMA NA HII  SALAH ANAWEZA KUSEPA LIVERPOOL