Home Simba SC MABAO 20 YAREJEA RASMI SIMBA

MABAO 20 YAREJEA RASMI SIMBA


CLATOUS Chama, mtambo wa mabao ndani ya Simba amerejea ndani ya kikosi cha Simba baada ya kuwa nje kwa muda kutokana na matatizo ya kifamilia.

Ndani ya Ligi Kuu Bara, Chama raia wa Zambia amehusika katika jumla ya mabao 20 kati ya 65 ambayo yamefungwa ndani ya mechi 28.

Chama alikuwa nchini Zambia baada  ya mkewe Mercy Mukuka kutangulia mbele za haki, Mei 29 hivyo hakuwepo katika mechi zilizofuata ndani ya Simba.

Alikosekana katika mchezo dhidi ya Namungo 1-3 Simba, Mei 29, Ruvu Shooting 0-3 Simba, Juni 3 na Polisi Tanzania 0-1 Simba, Juni 19.

Kupitia ukurasa wa Instagram wa Simba waeandika kwamba Amerudi, triple C.


SOMA NA HII  PAMOJA NA KUSHINDA MECHI..MASTAA SIMBA WACHIMBWA MKWARA...MATOLA AMNYOOSHEA KIDOLE BOCCO..