Home Yanga SC SARPONG , NCHIMBI KUIKAMUA YANGA BILIONI 4.9 KWA MISHAHARA TU

SARPONG , NCHIMBI KUIKAMUA YANGA BILIONI 4.9 KWA MISHAHARA TU


Klabu ya Yanga imetenga kitita cha Sh4.9 bilioni kwa ajili ya mishahara ya msimu wa 2021/2022.

Mbali na kitita hicho, pia imetenga bajeti ya Sh854.7 milioni ambayo ni kwa ajili ya bonusi.

Katika taarifa ya mapato na matumizi ambayo wanachama wa klabu hiyo wamepewa kwenye mkutano mkuu unaoendelea jijini Dar es Salaam, Yanga imeeleza kuwa inatarajia kukusanya Sh 8.1 bilioni kwenye vyanzo vyake vya mapato na matumizi yake ni Sh 7.9 bilioni.

Mkutano huo unaondelea leo Jumapili Juni 27, 2021 katika ukumbi wa DYCC jijini Dar es Salaam.

SOMA NA HII  BAADA YA KUWA KWENYE 'SONGOMBINGO' NA AZAM FC..YANGA WAMDAKA KININJA MUNATHIRI...ISHU IKO HIVI..