MWAKATALIMA, shabiki wa timu ya taifa ya Tanzania amesema kuwa ikiwa watatafutwa wachezaji wazuri kuna uhakika hapo baadaye kuwa na timu nzuri ya taifa. Jana Juni 13, Stars ilishinda mabao 2-0 dhidi ya Malawi katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Mkapa. Ameongeza kuwa kuna wachezaji wazuri ambao wanacheza Ligi Daraja la Kwanza na wanalijua lango kuliko akina Mbwana Samatta.