SENZO Mbata, Mshauri wa Klabu ya Yanga kuelekea katika mabadiliko amesema kuwa ushindi ambao waliupata mbele ya Ruvu Shooting wanaufurahia ila tabia ya Metacha Mnata haijawafurahisha. Jana Juni 17 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Ruvu Shooting 2-3 Yanga, Mnata alionekana akinyanyua dole kwa mashabiki jambo ambalo limewafanya viongozi wa Yanga kumsimamisha kwa muda usiojulikana