Home Azam FC CHAMA, BWALYA WAIPA AZAMA KIUNGO

CHAMA, BWALYA WAIPA AZAMA KIUNGO

 


KIUNGO mshambuliaji mpya wa klabu ya Azam, Charles Zulu amefunguka kuwa miongoni mwa sababu kubwa za yeye kusaini ndani ya kikosi cha Azam, ni kuvutiwa na viwango vya Clatous Chama, Rally Bwalya na Obrey Chirwa ambao ni raia wa Zambia wanaofanya vizuri hapa nchini.

Zulu alikamilisha usajili wake ndani ya kikosi cha Azam juzi Jumapili akitokea ndani ya klabu ya Cape Town City ya nchini Afrika Kusini, baada ya kufuzu vipimo vya afya.

Nyota huyo wa zamani wa wababe wa soka wa Zambia, klabu ya Zanaco amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Azam ambapo ataanza rasmi kutumika mwanzoni mwa msimu ujao wa Ligi Kuu Bara wa 2021/22.

Akizungumza baada ya kusaini Azam, Zulu amesema: “Nimefurahi kutua ndani ya kikosi cha Azam, kwangu hii ni hatua kubwa katika maisha yangu ya soka, na naamini nimekuja kuongeza thamani ndani ya timu hii. malengo yangu makubwa ni kushinda makombe.

“Nimevutiwa kujiunga Azam kwa sababu ya nafasi ya kushiriki michuano ya Afrika msimu ujao, lakini pia kutokana na mahusiano mazuri niliyonayo na baadhi ya wachezaji wa Zambia ambao wanafanya vizuri hapa Tanzania kama vile Clatous Chama, Rally Bwalya na Obrey Chirwa.”


 

SOMA NA HII  AZAM FC SERA YAO MPYA NI MWENDO WA KIMYAKIMYA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here