Home Simba SC KOCHA SIMBA ASEPA BONGO, KUKOSEKANA KWA MKAPA

KOCHA SIMBA ASEPA BONGO, KUKOSEKANA KWA MKAPA


SELEMAN Matola, Kocha Msaidizi wa Simba amesema kuwa leo pia Julai 7 mwalimu wa makipa Milton Nienov hatakuwepo kwenye bencho la ufundi baada ya kusepa Bongo.

Nienov raia wa Brazil, Julai 3 hakuwepo kwenye benchi ma ufundi na mikoba yake alikuwa nayo kipa namba moja Aishi Manula.

Ilikuwa ni kwenye mchezo wa Kariakoo Derby baada ya dk 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Simba 0-1 Yanga huku bao la ushindi likipachikwa na Zawad Mauya. 

Kwa mujibu wa Matola amesema kuwa kocha huyo anasoma hivyo kipindi hiki ni cha mitihani.

SOMA NA HII  KIPA MPYA SIMBA MAMBO BADO