MABINGWA wa Kombe la Shirikisho, Simba tayari wameshawasili Dar na taji hilo baada ya kulitwaa jana.
Katika mchezo wa Kombe la Shirikisho kwenye fainali walikutana na Yanga ambao ni watani zao wa jadi.
Ushindi wa bao 1-0, Uwanja wa Lake Tanganyika kupitia kwa Taddeo Lwanga ulitosha kuwafanya watetee taji hilo.
Ikumbukwe kwamba walitwaa msimu wa 2019/20 zama za Sven Vandenbroec, Sumbawanga kwa ushindi mbele ya Namungo na jana ilikuwa mbele ya Yanga.
Kocha wa sasa ambaye ni Didier Gomes amesema kuwa ni furaha kwake kuona wanatimiza lengo ambalo walijiwekea.