RAZACK Siwa, Kocha wa Makipa amesema kuwa timu ya Yanga ni bora na inawachezaji wazuri watakaoipa matokeo chanya.
Kesho Julai 3, Yanga itakuwa na kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Simba katika mchezo wa ligi.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Siwa amesema kuwa wanaamini uimara walio nao hivyo watapambana kupata matokeo mbele ya Simba.
“Moja ya timu bora na Yanga pia ni mojawapo hivyo kuelekea katika mchezo wetu dhidi ya Simba hatuna mashaka.
“Imani yetu nikuona kwamba tunapata ushindi, mashabiki wajitokeze kwa wingi ili kutupa sapoti,” amesema.
Katika mchezo wa mzunguko wa awali, ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Yanga 1-1 Simba ambapo watupiaji walikuwa ni Michael Sarpong na Joash Onyango.
Katika msimamo Yanga ipo nafasi ya pili na ina pointi 67 huku Simba ikiwa nafasi ya kwanza na pointi 73.
Yanga inapambana kurejesha nguvu ya kutwaa ubingwa pamoja na kuwania nafasi ya pili huku Simba ikihitaji pointi tatu kutangazwa kuwa mabingwa mara ya nne mfululizo.