Home Simba SC PETER BANDA AITWA TIMU YA TAIFA YA MALAWI

PETER BANDA AITWA TIMU YA TAIFA YA MALAWI


 BAADA ya kumaliza maandalizi ya kwanza kuelekea msimu mpya wa 2021/22 na kurejea Tanzania, kiungo  wa Simba Peter Banda ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Malawi.

Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes iliweka kambi kwa muda nchini Morocco kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.

Banda ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Malawi kwa ajili ya kujiandaa na michezo ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia nchini Qatar mwaka 2022. 

Pia wapo nyota wengine wa Simba ambao wapo kwenye kambi ya timu ya taifa ya Tanzania ambao ni pamoja na Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohamed Hussein pamoja na John Bocco.


SOMA NA HII  BAADA YA KUZUIWA KUINGIA UWANJANI NA PABLO..WAWA AVUNJA UKIMYA ..AFUNGUKA YANAYOENDELEA...