Home news YANGA KAMILI KUKWEA PIPA KUWAFUATA RIVERS UNITED

YANGA KAMILI KUKWEA PIPA KUWAFUATA RIVERS UNITED


KIKOSI cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi leo kinakwea pipa kueleka Nigeria kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Huu ni mchezo wa marudio wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Rivers United baada ya ule mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Mkapa ubao kusoma Yanga 0-1 Rivers United. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Ofisa Habari wa Yanga, Haji Manara amesema kuwa wanakwenda kufanya kazi kubwa na wataongea na wachezaji ili waweze kupigana kwa jasho jingi.

“Mchezo  utakuwa mgumu lakini tupo tayari kwa kuwa tutakuwa ndani ya ndege binafsi tutazungumza na wachezaji wakapambane kwa jasho jingi,”.

SOMA NA HII  TWIGA STARS YATINGA FAINALI COSAFA