Home news BAADA YA KUTOSWA KWENYE TUZO ZA TFF…MORISSON AIBUKA NA TUZO YAKE BINAFSI…ATAMBA...

BAADA YA KUTOSWA KWENYE TUZO ZA TFF…MORISSON AIBUKA NA TUZO YAKE BINAFSI…ATAMBA NAYO BALAAH


Wakati wachezaji John Bocco, Aishi Manula, Mohammed Hussein na Fei Toto kuondoka na tuzo za TFF usiku wa jana, Benard Morrison anasema aliambulia kurudi na chupa ya maji nyumbani.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram mchezaji huyo asiyeishiwa na vituko ameandika kuwa tuzo pekee aliyoshinda ni nguo bora ya ndani ya msimu.

“Kwa hivyo jana usiku wengine walipokwenda nyumbani na tuzo, mimi nilikwenda nyumbani na chupa ya maji, lazima nikuambie kabla ya kuanza kusema nimeshinda nguo bora ya ndani ya msimu, kila mtu alistahili hongera kwa wote”.

SOMA NA HII  WAZEE WA 5G LEO MZIGONI TENA....RATIBA YA MECHI ZOTE ZA MAPINDUZI CUP LEO HII HAPA...