Home news SIKU KADHAA KABLA YA KUKUTANA NA YANGA…KAGERE AIBUKA NA JIPYA SIMBA…AGUSIA MAKOSA…

SIKU KADHAA KABLA YA KUKUTANA NA YANGA…KAGERE AIBUKA NA JIPYA SIMBA…AGUSIA MAKOSA…


 MSHAMBULIAJI wa Simba Meddie Kagere amesema michezo miwili mikubwa ijayo ya timu hiyo wanaichukulia kama fainali na watapambana mpaka tone la mwisho uwanjani dhidi ya Red Arrows na Yanga.

Kagere alisema wanatambua uzito kwa kila mchezo ingawa kwa sasa akili zao wamezielekeza kwenye mechi na Red Arrows ili kufanya vizuri na kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

β€œKuanzia viongozi, benchi letu la ufundi na wachezaji tumejiandaa vyema kufanya vizuri maana tunatambua umuhimu wa mchezo huo hivyo hatutaki kurudia tena makosa ambayo yalitokea mwanzo,” alisema.

β€œKila mchezo kwetu ni fainali, tunajua wengi wanaangalia sana mechi ya Yanga kutokana na ukubwa na historia ya timu hizi lakini tunaenda hatua kwa hatua na zamu yao itafika baada ya kutoka Zambia,” alisema Kagere ambaye ni raia wa Rwanda mwenye asili ya Uganda.

Akiwa na kikosi hicho msimu huu kwenye michezo ya Ligi Kuu Bara amefunga mabao manne kwenye chati ya wafungaji bora nyuma ya kinara wa mabao Jeremiah Juma wa Tanzania Prisons mwenye mabao matano.

Alifunga bao moja kwenye ushindi dhidi ya Dodoma Jiji na Namungo FC huku akitupia mabao mawili kwenye ushindi wa 3-1, dhidi ya Ruvu Shooting.

SOMA NA HII  DAKTARI WA VIUNGO YANGA AKOMAA NA MAXI ISHU IKO HIVI