Home Uncategorized TFF ULINZI WAO LEO SI MCHEZO, KISA ISHU YA MORRISON

TFF ULINZI WAO LEO SI MCHEZO, KISA ISHU YA MORRISON

 

Makao makuu ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) hali ni ya utulivu kabisa huku ulinzi ukiwa umeimarishwa.

Inaelezwa kuwa Bernard Morrison kiungo wa Yanga yupo kwenye kikao na viongozi wa TFF kuhusu suala la mkataba wake muda huu.

Pia wapo viongozi wa Simba na wale wa Yanga na ulinzi uliowekwa makao makuu sio wa mchezo.

Lilipita ndiga ya Polisi ikiwa imebeba Polisi na kuingia ndani kisha baada ya muda ilitoka na getini umewekwa ulinzi ambao haujawahi kuwepo siku za hivi karibuni ndani ya TFF.

Getini yupo Polisi mmoja kamanda wa kazi ambaye kabla hujapita getini anakuhoji namna hii:”Unakwenda kwa nani? Je una appointment naye? Ohh waandishi wa habari haturuhusu waandishi kuingia,”.

SOMA NA HII  WAGOSI WA KAYA NAO HAWAKO NYUMA WAANZA HIVI KWENYE DIRISHA DOGO LA USAJILI