Home Makala BILA WAO KUJIJUA….HUYU HAPA ‘BUNDI’ ANAYENING’INIA KWENYE VIUNGA VYA MSIMBAZI..PABLO HOI….

BILA WAO KUJIJUA….HUYU HAPA ‘BUNDI’ ANAYENING’INIA KWENYE VIUNGA VYA MSIMBAZI..PABLO HOI….


Bundi ni ndege ambaye anatajwa kua na mikosi sana ulimwengu huu, jamii nyingi zimekua na imani tofauti tofauti juu ya ndege huyu ambaye wakati mwingine amekua akitumiwa kwenye masuala ya ushirikina.

Klabu ya Simba Sc wameendelea kupata matokeo mabovu kwenye msimu huu mara baada ya kukubali kufungwa na klabu ya Kagera Sugar kwenye uwanja wa Kaitaba uliopo mkoani Kagera. Goli pekee katika mchezo huo limefungwa na aliyekua mshambuliaji wa vilabu vya Simba Sc na Yanga Hamis Kiiza raia wa Burundi.

Klabu ya Simba Sc wanapitia wakati mgumu sana siku za hivi karibuni ikiwa ni pamoja na kupata matokeo mabaya kwenye michezo yao mitatu iliyopita. Simba Sc wameambulia alama moja pekee kwenye michezo mitatu iliyopita ambapo walitoa sare dhidi ya ya Mtibwa Sugar, na wamepoteza michezo miwili dhidi ya Mbeya City na Kagera Sugar.

Takwimu hizo kwa klabu ya Simba Sc ni mbaya sana ulizingatia malengo yao msimu huu ambapo wamepanga kushinda ubingwa wa NBC Premier League. Mambo yanazidi kua magumu kwa klabu ya Simba Sc kwa sababu mpaka sasa watakua wanazidiwa alama 10 na wapinzani wa Yanga ambao wanaongoza katika msimamo wa ligi.

Simba Sc wameingia kwenye wimbi zito la mikosi kiasi kwamba wanapoteza mvuto wa timu hiyo kama ilivyokua misimu kadhaa iliyopita ambapo waliweka rekodi ya kushinda taji la ligi kuu Tanzania bara kwa misimu minne mfululizo.

Simba Sc wanapotea kwenye ramani na sasa baadhi ya mashabiki wa soka nchini Tanzania wameanza kutoa utabiri wao juu ya nafasi ya timu hii katika mbio za ubingwa.

Tatizo la kufunga magoli kwa safu ya ushambuliaji wa klabu ya Simba Sc linazidi kukua siku hadi siku na hii imekua ndio sababu kubwa kwa timu hiyo kupata matokeo mabaya kwenye michezo ya hivi karibuni.

Pablo Franco amefanya jitihada zake za kuhakikisha kwamba timu inapata matokeo lakini jitihada hizo ni kama zimegonga mwamba na sasa Simba Sc wanaendelea kusota kwa kupata matokeo mabaya.

SOMA NA HII  KISA KUHOJI HOJI SANA KUHUSU BIL 20 ZA MO DEWJI...SIMBA WAMSHUKIA JUMLA JUMLA DK KIGWANGALLA...

Wachezaji wa Simba Sc wanatengeneza nafasi nyingi za wazi lakini suala la kufunga magoli imekua changamoto kubwa sana wa wachezaji wote. Bwalya, Sakho, na Mzamiru Yassin wamepata nafasi za wazi lakini wameshindwa kupata magoli kwenye mchezo  ambao ulikua muhimu sana kwa upande wao.