Home news KUELEKEA MECHI DHIDI YA NAMUNGO…PABLO AVUNJA UKIMYA SIMBA..AFUNGUKA ‘NJAA’ WALIYONAYO…

KUELEKEA MECHI DHIDI YA NAMUNGO…PABLO AVUNJA UKIMYA SIMBA..AFUNGUKA ‘NJAA’ WALIYONAYO…


PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa wamechagua kuwapa furaha mashabiki wa timu hiyo hivyo kesho watafanya vizuri kusaka ushindi.

Leo Januari 10 Simba itakuwa na kibarua kwenye Kombe la Mapinduzi ambapo inatarajia kumenyana na Namungo FC kwenye mchezo wa hatua ya nusu fainali.

Mchezo wake uliopita ilitoshana nguvu na Mlandege na dakika 90 zilikamilika kwa ubao wa Uwanja wa Amaan kusoma Simba 0-0 Mlandege.

Pablo amesema:”Tunajua kwamba utakuwa mchezo mgumu hasa ukizingatia kwamba timu ambayo tunakutana nayo inahitaji pia ushindi hamna namna lazima tuwe na mbinu ya kipekee.

“Kwetu utakuwa ni mchezo mgumu lakini tutajaribu kucheza mchezo wetu bora kwa sababu tumekuja hapa kuwapa furaha mashabiki,” ,

SOMA NA HII  UKUTA WA SIMBA WAWEKA REKODI MPYA BONGO..ONYANGO NA WAWA WATAJWA