Home news PAMOJA NA KUTEMWA YANGA …NYOTA YA KABWILI YAZIDI KUWAKA…AKIMBILIWA NA MBEYA CITY..

PAMOJA NA KUTEMWA YANGA …NYOTA YA KABWILI YAZIDI KUWAKA…AKIMBILIWA NA MBEYA CITY..


UKISEMA wa nini wenzako wanajiuliza watampata lini. Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mbeya City ambapo inaelezwa kuwa imeonyesha nia ya  kumsajili aliyekuwa  kipa namba tatu wa Yanga, Ramadhan Kabwili.

Chanzo kutoka Yanga, kimesema kuwa: “Wakati viongozi  walipokuwa  katika mchakato wa kumuondoa Ramadhan Kabwili kikosini, kuna klabu ya ligi kuu ilikuwa  imetuma barua ya kuhitaji huduma yake.

“Barua ililetwa Jangwani kutoka Klabu ya Mbeya City ambayo imeonesha nia ya dhati kabisa ya kuhitaji huduma ya Kabwili.

Alipotafutwa Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli kuzungumzia hilo, alisema: “Masuala ya usajili yatakapokamilika yatawekwa wazi na klabu, lakini mpaka sasa tumeshamtangaza wachezaji tuliosajili na kuwaacha”.

SOMA NA HII  DILI LA YANGA NA NMB USIPIME....ACHANA NA KADI TU..ISHU YA UWANJA NA MENGINE YAKO HIVI...