Home news WAKATI WATU WAKILALAMIKA KUHUSU PENATI YA SIMBA..KOCHA WA TZ PRISONS AAMUA KUIBUKA...

WAKATI WATU WAKILALAMIKA KUHUSU PENATI YA SIMBA..KOCHA WA TZ PRISONS AAMUA KUIBUKA NA HILI JIPYA…


SHABAN Kazumba, Kocha Msaidizi wa Tanzania Prisons, amesema kuwa bao la penalti ambayo walipata Simba juzi ni halali kwa kuwa ilitolewa na mwamuzi kutokana na makosa ambayo walifanya.

Bao hilo lilifungwa na Meddie Kagere na lilionekana kuwa na utata kutokana na wachezaji wa Prisons kumfuata mwamuzi kulalamika juu ya penalti hiyo.

Kazumba aliliambia gazeti la Championi Jumamosi kuwa: “Simba wamepata penalti, kwangu penati ni sehemu ya makosa, siwezi kusema kwamba tumefungwa kwa bao la penalty, hapana, siwezi kusema kwamba namlaumu mwamuzi.

“Kwangu naona liko sahihi lakini kidogo naona ilikuwa ni kwa wepesi kwetu, lakini tumefungwa, tunakubali matokeo, tumepoteza pointi tatu na timu yangu ilicheza mpira ule unaopendwa na Kocha Mkuu, Patrick Odhiambo ambaye anapenda kuona timu inacheza mpira mzuri.

“Tulikosa nafasi tatu za kufunga mbele ya Simba na tulikuwa tunajua kwamba tunacheza na mabingwa, Simba alistahili na mchezo wa mpira ni mgumu sana.”

Prisons ipo nafasi ya 16 ikiwa na pointi 11 huku Simba ikiwa nafasi ya pili na pointi 28, zote zimecheza mechi 14.

SOMA NA HII  BAADA YA KUNUSURIKA KUSHUKA DARAJA ...KOCHA MTIBWA SUGAR AKATAA USAJILI WA WACHEZAJI VIBABU...