Home Habari za michezo CAF YAIPIGA RUNGU LA ADHABU SIMBA KWA KUFANYA “TAMBIKO LA KISHIRIKINA” UWANJANI….

CAF YAIPIGA RUNGU LA ADHABU SIMBA KWA KUFANYA “TAMBIKO LA KISHIRIKINA” UWANJANI….


Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limeipiga faini ya Dola za Marekani 10,000 (zaidi ya Tsh. Milioni 23) Klabu hiyo baada ya kupatikana na hatia ya kufanya ‘tambiko hatarishi’ katika mchezo dhidi ya Orlando Pirates.

Kabla ya mchezo huo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho, Wachezaji wa Simba walionekana kukusanyika katikati ya uwanja na baadaye moshi kutokea katikati ya kundi hilo

Taarifa kutoka CAF imesema Maafisa wa mchezo walionesha katika ripoti zao kwamba “Wachezaji wa Simba waliwasha moto katikati ya uwanja wakati wakijifanya kuomba kabla ya mechi. Ilitubidi kumwaga maji ili kuuzima moto”

SOMA NA HII  USHIRIKINA WAIPONZA TIMU YA MASHUJAA FC, WAPIGWA FAINI HII

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here