Home CAF BAADA YA KUFUKUZWA NA AL AHLY….RAIS WA CAF AIBUKA NA HILI KUHUSU...

BAADA YA KUFUKUZWA NA AL AHLY….RAIS WA CAF AIBUKA NA HILI KUHUSU PITSO MOSIMANE….ADAI ATAMLIPA MSHAHARA YEYE…


Rais wa shirikisho la soka Afrika CAF na mmiliki wa klabu ya Mamelodi Sundowns Patrice Motsepe, amesema yuko tayari kumlipa mshahara kocha Pitso Mosimane ikiwa ataifundisha timu ya taifa ya Afrika Kusini ‘Bafana Bafana’

Pitso Mosimane hivi karibuni ameacha kazi kwenye klabu ya Al Ahly, baada ya kudumu kwa muda wa miaka miwili na kufanikiwa kushinda makombe mawili ya klabu bingwa barani Afrika, ligi kuu ya Misri na kombe la Super Cup Afrika, huku akiacha historia ya kucheza fainali tatu za ligi ya mabinga Afrika.

Akiwa kwenye kongamano la SAEditorsForum nchini Afrika Kusini alielezea hisia zakw kwa kocha anayempenda na kunukuliwa, β€œbila shaka kocha ninayempenda ni Pitso, nampenda sana pitso na nitampenda daima, anasehemu maalum kwenye moyo wangu.

SOMA NA HII  STRAIKA LA MABAO SIMBA QUEENS AGOMBANIWA ULAYA...MWENYEWE KAANIKA HAYA...