Home Habari za michezo BADO LA KIDEONI ALILOFUNGA SAKHO LAPETA AFRIKA…CAF WALITAJA KWENYE MABAO BORA YA...

BADO LA KIDEONI ALILOFUNGA SAKHO LAPETA AFRIKA…CAF WALITAJA KWENYE MABAO BORA YA MSIMU…


Bao la la acrobatic alilowafunga ASEC Mimosas katika mchezo wa hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho Afrika limechaguliwa kuingia 10 Bora barani Afrika likishindania bao bora la mwaka.

Sakho alifunga bao hilo katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar akimalizia mpira wa krosi uliopigwa na beki wa kulia Shomari Kapombe.

Mchezo huo ambao ulikuwa wa kukata na shoka ulipigwa Februari 13, 2022. Simba iliishia hatua ya robo fainali katika michuano ya Shirikisho Afrika baada ya kupigwa kwa mikwaju ya penalti katika mechi ya marudiano ya robo fainali kule Afrika Kusini ambapo Orando Pirates walifanikiwa kufunga 4 kwa 3.

SOMA NA HII  KUELEKEA MICHUANO YA KLABU BINGWA AFRIKA....CAF WASHUSHA WARAKA HUU KWA SIMBA NA YANGA...