Klabu ya Coastal Union imetangaza kutokuwa na mkataba na Kocha Juma Mgunda ambaye kwa sasa anaitumikia Simba akiwa kocha wa muda.
Coastal imeeleza mazungumzo ya kusaini mkataba mpya baina yao na Mgunda yalikuwa kwenye mchakato, hivyo suala la Mgunda kujiunga na Simba ni la kwake binafsi.
Kutokana na hali hiyo uongozi wa Coastal Union umemtangaza Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Joseph Lazaro kusimamia timu kwa muda.
Taarifa ya Coastal Union hii hapa chini.