Home Habari za michezo KUWANIA LIGI YA MABINGWA AFRIKA KWA WANAWAKE…SIMBA QUEENS WAIZIDI KUTIKISA AFRIKA…

KUWANIA LIGI YA MABINGWA AFRIKA KWA WANAWAKE…SIMBA QUEENS WAIZIDI KUTIKISA AFRIKA…


SIMBA Queens leo imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Corporate FC kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa  ukanda wa CECAFA kwa Wanawake uliochezwa Uwanja wa Azam Complex.

Mchezo huo ni wakuwania kupata nafasi ya kufuzu mashindano hayo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa dk zote 90.

Mabao ya Simba yamefungwa na Aquino Corazone dk ya 21 akitumia pasi ya Bukulu aliyepiga faulo  na Pambani Kuzoya alipachika bao dk ya 61.

Simba wameendeleza ushindi jambo ambalo linawapa nguvu ya kuweza kusonga mbele hatua inayofuata ya robo fainali

SOMA NA HII  YANGA NGUVU ZAO KWA GEITA GOLD