Home Habari za michezo MKATABA WA SIMBA NA M-BET WAMTIA JEURI YA MANENO AHMED ALLY…AWAPIGA KIJEMBE...

MKATABA WA SIMBA NA M-BET WAMTIA JEURI YA MANENO AHMED ALLY…AWAPIGA KIJEMBE CHA MWAKA YANGA….


Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Ahmed Ally amesema Simba ya sasa haitofanana kitu chochote na klabu nyingine ya Ligi Kuu kuanzia msimu ujao.

Ahmed amesema hayo wakati wa utambulisho rasmi wa mdhamini mkuu wa klabu hiyo kampuni ya M-bet.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Ahmed amesema zamani Simba ilikuwa inafanana kila kitu lakini safari hii itakuwa tofauti.

“Zile zama za kuwa na mikataba sare sare imeshapita, sisi Simba tunahitaji vitu vya tofauti kwa sababu tumewekeza kwa kiasi kikubwa,” amesema Ahmed.

Ahmed amesema hawana muda wa kuficha ficha masuala ya mikataba yao na ndio maana leo wameweka wazi.

“Tulisema leo tutaweka wazi kila kitu wakati tunatangaza wadhamini wetu na leo tupo hapa kuweka wazi mkataba una thamani gani,”

Simba na Yanga kwa miaka ya nyuma Simba na Yanga zilikuwa zinafanana kwenye mikataba ya kampuni zinazowadhamini.

Awali mwezi uliopita Simba iliitangaza M-Bet kuwa mdhamini mkuu baada ya kumaliza mkataba wao na kampuni ya SportPesa.

SOMA NA HII  MASTAA YANGA WAPIGWA MKWARA....