Mchezaji Singida Big Stars afariki dunia
Habari za michezo

HIZI HAPA SABABU YA KIFO CHA MCHEZAJI WA U17 WA SINGIDA BIG STAR ALIYEFIA UWANJANI LEO..

admin January 19, 2023 7:59 pm

Kinda wa Singida Big Stars aliyefia uwanjani, Mohammed Banda anatarajiwa kuzikwa kesho saa saba mchana katika kijiji cha Mlandala wilayani Iramba mkoani Singida.

Banda alifariki mapema leo asubuhi wakati kikosi cha timu ya vijana U17 kikifanya mazoezi katika uwanja wa Magereza mkoani Singida.

Kinda huyo ambaye ni nahodha wa kikosi hicho alikuwa akigombea mpira wa juu na mshambuliaji wa timu hiyo.

Mtendaji Mkuu wa timu hiyo,Muhibu Kanu amesema kama timu wamechukua majukumu yote kuhakikisha wanamstiri mchezaji huyo na anapata heshima zote.

Amesema marehemu atazikwa kesho katika kijiji cha Mlandala wilayani Iramba mkoani Singida.

“Kesho tutatoka hapa kwenda nyumbani kwao kule Mlandala njia ya kwenda Iramba ataenda kuzikwa saa saba kamili,”amesema Muhibu.

Akisimulia jinsi ilivyokuwa Muhibu amesema kocha wa timu ya vijana aitwaye Mtipa aliamua kuweka full game ili kuangalia kile ambacho amefundisha.

“Kwenye kucheza kulikuwa na defender na striker imewekwa krosi,striker kaweka kichwa kufunga na defender kama kawaida anataka kuokoa, kwenye kuokoa wakagongana hewani,”amesema

Amesema baada ya kugongana wakaanguka chini lakini aliyeanguka vibaya zaidi ni defender ambaye ni Banda.

“Akapata huduma haraka haraka ukafanyika utaratibu wa kumpeleka hospitali na sisi tukapigiwa simu tukawahi tukamchukua tukampeleka hospitali, madaktari wamefanya kazi yao nzuri lakini wamejitahi kuokoa lakini tukampoteza,”amesema Muhibu.

AUCHO NI MAJANGA JUU YA MAJANGA YANGA….ISHU NZIMA IKO HIVI… WAKATI MASHABIKI SIMBA WAKILIA NA ‘SUB’ YA CHAMA…MBRAZILI KAWASIKIA..KISHA AKAJIBU HIVI..

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply