Home Habari za michezo BAADA YA KUCHEMSHWA NA ISHU YA CHAMA….KIGINGI KINGINE CHA MBRAZILI SIMBA HIKI...

BAADA YA KUCHEMSHWA NA ISHU YA CHAMA….KIGINGI KINGINE CHA MBRAZILI SIMBA HIKI HAPA…

Habari za Simba SC

Kikosi cha Simba SC leo Jumamosi, Januari 21, 2023 asubuhi kimerejea tena mazoezini kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Dodoma Jiji utakaopigwa Jumapili Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mbeya City wachezaji wa Simba walipewa mapumziko ya siku moja na kesho wachezaji watarejea mazoezini.

Wachezaji wapya waliosajiliwa katika dirisha hili Hamed Ismael Sawadogo, Jean Baleke na Mohamed Mussa watashiriki mazoezi hayo.

Inadaiwa kuwa Kama Kocha Mkuu Roberto Oliviera ‘Robertinho’ na wasaidizi wake wataona inafaa wanaweza kuwatumia katika mchezo huo kwa kuwa masuala yao ya vibali tayari yamekamilika.

SOMA NA HII  WADAU WA SOKA LA BONGO WATAKA KOCHA MPYA WA SIMBA APIMWE HIVI