Home Habari za michezo SIMBA vs AL HILAL….MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA LEO NI HAYA….

SIMBA vs AL HILAL….MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA LEO NI HAYA….

Simba vs Al Hilal leo

Mchezo wa kirafiki baina ya Simba SC dhidi ya Al Hilal utakuwa kipimo kizuri kwa Mnyama kuelekea mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika watakapo wakabili Horoya itakayopigwa Februari 11.

Al Hilal ni moja ya timu Bora barani Afrika ambapo itatoa mwangaza wa hali ya ubora wa kikosi cha Simba kuelekea mchezo wa Horoya.

Al Hilal nayo inayojiandaa kwa mchezo wao na Mamelodi Sundowns itakuwa imepata maandalizi mazuri kwa mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa.

Kocha wa Al Hilal, Florent Ibenge anauchukulia mchezo huo kama wa Ligi ya Mabingwa Afrika kwakuwa anaenda kukutana na timu bora zaidi.

SOMA NA HII  KISA TABIA ZA 'KITOTO' ...MASTAA YANGA WAMSHUKIA MORRISON...WAMPA 'MAKAVU LIVE'...