Tetesi za Usajili Yanga
Habari za michezo

KUHUSU UKWELI WA FEI TOTO KULA UGALI NA SUKARI….MAMA YAKE AANIKA UKWELI WOTE HADHARANI…

admin March 3, 2023 9:38 am

Mama mzazi wa aliyekuwa mchezaji wa Yanga, Feisal Salum ‘Fei Toto’ amnedai kuwa mwanaye huyo amenyanyasika akiwa ndani ya Klabu hiyo ndiyo maana akaamua kuomba haki yake.

“Fei amedharirika sana mpaka hapa ilipofikia sasa ndio maana nimeona sio wakati wa kuficha ni bora niweke hadharani. Naomba TFF huyu mtoto imtendee haki yake, Fei imefika wakati wakati akawa anakula ugali na sukari, leo ndiyo nasema sasa. Kwa kutetea haki yake lakini alikuwa anaficha.

“Feisal ni mchezaji wa taifa, leo amekaa kama mtu aliyeua wakati anadai haki yake. Ilifika wakati anakwenda kwenye mazoezi na bodaboda na pesa ya kumlipa hana lakini kwa vile anafahamiana naye anamkopa.

“Inafika wakati anakosa hata pesa ya matumizi ananipigia simu kuniomba na mimi ninamtegemea yeye mengine siwezi kuyasema. Alikuwa anajituma kwa sababu ya ndugu zake.

“Nataka TFF wasome shitaka la Fei walisome kwa Kiswahili ili kila mtu ajue aliyoyapitia. Fei sasa hivi hana furaha na Yanga bora aondoke tu, mtoto kateseka sana. Amepambana kwa njia za kawaida kuwaomba wamuongezee maslahi yake lakini wakaona hana thamani,” amesema Mama Fei.

Ikumbukwe kuwa, Fei aliandika barua kuomba kuondoka Yanga lakini klabu iligoma hivyo akaamua kuondoka klabuni hapo.

Kufuatia jambo hili, Yanga walifungua shauri TFF ambapo baada ya vikao vingi jana Kamati ya Hadhi na haki ya wachezaji ya TFF ilimuidhinisha Feisal Salum, kuwa mchezaji wa Yanga.

JULIO;- SIMBA NIPENI KAZI MFURAHI…YANGA WANAFANIKIWA KWA SABABU YA WATU KAMA SISI… SIKU KADHAA BAADA YA KUHAMA YANGA….YACOUBA NAYE ATEMA NYONGO…AMTAJA OKRAH WA SIMBA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply