Home Habari za michezo BAADA YA FEI TOTO KUTAKA KUVUNJA MKATABA YANGA…NABI AIBUKA NA MSIMAMO HUU...

BAADA YA FEI TOTO KUTAKA KUVUNJA MKATABA YANGA…NABI AIBUKA NA MSIMAMO HUU JUU YAKE..

Habari za Yanga

Baada ya kumkosa Kiungo wake kwa muda sasa, Kocha wa Yanga, Nasreddine Nabi ametoa neno kwenda kwa kiungo huyo aliekuwa mhimili muhimu ndani ya kikosi cha Yanga.

Akizungumza Nabi juu ya mustakabali wa Fesal Salum ambae amefanya nae kazi kwa misimu zaidi ya miwili nabi amesema

“Feisal Salum ni kama mwanangu, napenda arejee kwenye timu na majukumu yake ya kawaida. Nikipewa nafasi ya kumshauri ningemshauri arudi hapa. Nitampokea kwa mikono miwili. Kama anaona hakuna haja ya kurejea basi namtakia kila la kheri kwenye safari yake”

Feisal anapambana katika mamlaka za soka nchini ili kuvunja Mkataba wake na Klabu ya Yanga.

Ambapo hivi karibuni alirudisha shauri tena TFF kuomba mkataba wake uvunjwe, ikiwa ni siku chache baada ya Kamati kumrudisha Yanga kupitia shauri la awali.

SOMA NA HII  ROBERTINHO APATA DAWA YA WAZAMBIA ISHU IKO HIVI