Home Habari za Simba MNAWASIFIA SANA MAMELODI SUNDOWNS…WATAPIGWA NA SIMBA MSHANGAE

MNAWASIFIA SANA MAMELODI SUNDOWNS…WATAPIGWA NA SIMBA MSHANGAE

MNAWASIFIA SANA MAMELODI SUNDOWNS...WATAPIGWA NA SIMBA MSHANGAE

Awali ya yote ningependa ku-declare interest kuwa nawataka Masandawana.

Twende kwenye mada, imezuka mijadala mingi sana mitandaoni hususani kwa baadhi ya wachambuzi wakisema kuwa Mamelodi sundowns sio timu ya kuomba kukutana nayo. Wengine wakaenda mbali zaidi kusema kuwa ndio timu hatari zaidi.

Binafsi naheshimu ubora wa Mamelodi, nilipata wasaa wa kutizama game zao mbili tatu hususani ile game yao ambayo walimpiga Al ahly hamsa pale Africa kusini. Naomba niseme tu kwamba Mamelodi wako Overrated mno.

Nadhani ni kwa sababu ya kumnyanyapaa Al ahly ndicho kinachofanya watu wamzungumzie kiutofauti, ambapo obviously hajaanza leo toka kitambo al ahly anapotua Johannesburg basi Hamsa zina muhusu.

Lakini ni ukweli usiopingika kuwa al ahly pia msimu huu hayupo vizuri, kinacho mbeba ni uzoefu tu ila hana timu, nisingeshangaa angepigwa nje ndani na mnyama simba kama angepangwa group moja.

Turudi sasa kwenye mada yetu, Mamelodi sundowns pamoja na kuwa Overrated sana bado hana mpira wa kutisha, nachelea kusema kuwa hata Raja CA ni maji marefu kwa Mamelodi. Kingine nilichokiona kwa Mamelodi ni aina yao ya uchezaji ambao uko very identical na uchezaji wa simba yani pira biriani a.k.a Sambaloketo.

Hivyo ikitokea timu hizi mbili zikakutana, basi Africa na Dunia kiujumla itashuhudia mechi ya karne, yani historical match, hivyo niwatoe hofu wanasimba wenzangu ambao mmeanza kutishika na maneno ya waganga njaa kuhusu Mamelodi sundowns.

Binafsi sintoshangaa kabisa kama simba akimtoa Sundowns kwenye hatua ya Robo fainali au hatua yoyote tutakayo kutana nae.

Nguvu moja

SOMA NA HII  STAA YANGA:- MAYELE AKIACHA UCHOYO TUTASHINDA...USILAZIMISHE KUFUNGA TOA PASI