Home Habari za michezo ILI KUWAMALIZA KABISA WANIGERIA…MAYELE AWEKEWA MIL 300 CASH MEZANI….

ILI KUWAMALIZA KABISA WANIGERIA…MAYELE AWEKEWA MIL 300 CASH MEZANI….

Habari za Yanga SC

Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya uongozi wa Yanga SC zinaeleza kuwa mabosi wa timu hiyo wameweka ahadi ya Sh 300 Mil kwa wachezaji na benchi la ufundi endapo watafanikiwa kuibuka na ushindi katika mchezo wa marudiano vs Rivers United kwa Mkapa.

Yanga SC katika mchezo huo kama watapata ushindi watajihakikishia nafasi ya kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho na kuweka rekodi jambo ambalo mabosi wa Yanga wanataka kuona hilo likitimia ndio maana wameweka ahadi hiyo.

Mchezo huo wa pili wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika unatarajiwa kuchezwa Jumapili hii, Aprili 30, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.

SOMA NA HII  WALICHOSEMA WACHAMBUZI WAKIFARANSA WAKATI WAKIMCHAMBUA MAYELE....ABATIZWA JINA JIPYA....