Home Habari za michezo KIKOSI CHA SIMBA SAFARINI KUELEKEA MOROCCO…WATUMIA MBINU HII KUWACHANGANYA WAARABU

KIKOSI CHA SIMBA SAFARINI KUELEKEA MOROCCO…WATUMIA MBINU HII KUWACHANGANYA WAARABU

KIKOSI CHA SIMBA SAFARINI KUELEKEA MOROCCO...WATUMIA MBINU HII KUWACHANGANYA WAARABU

Kikosi cha Simba kinaondoka jijini Dar es salaam leo kuelekea Morocco kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Wydad Athletic.

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema msafara unaoelekea Morocco utakuwa wa awamu mbili.

Awamu ya kwanza imeondoka JANA saa mbili usiku ukijumuisha watu 29 wakiwa ni wachezaji na benchi la ufundi.

Kikosi kimefika Dubai. Safari itaendelea saa 1:45 asubuhi kuelekea Casablanca kwa kupitia Tunis.

Msafara wa pili utaondoka Jumanne, utajumuisha watu 20, wakiwa ni viongozi na kiongozi wa msafara kutoka TFF.

Ahmed amesema Simba inakwenda Morocco kupambana
kuhakikisha wanapata matokeo yatakayowapeleka nusu fainali siku ya Ijumaa, April 28.

SOMA NA HII  LUIS, LWANGA,CHAMA MIKONONI MWA AL AHLY, KOCHA AWATAJA