Home Habari za michezo KIPA CHIPUKIZI SIMBA AMWAGA SIRI NZITO…AMTAJA AISHI MANULA…ISHU IKO HIVI A-Z

KIPA CHIPUKIZI SIMBA AMWAGA SIRI NZITO…AMTAJA AISHI MANULA…ISHU IKO HIVI A-Z

KIPA CHIPUKIZI SIMBA AMWAGA SIRI NZITO...AMTAJA AISHI MANULA...ISHU IKO HIVI A-Z

KIPA chipukizi wa Simba, Ally Salim amesema kuwa licha ya kuwa namba tatu na kukosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza lakini alikuwa anajiandaa vizuri ili kukabiliana na dharura yoyote ambayo ingetokea.

Salim alidaka kwenye dabi ambapo Simba iliondoka na ushindi wa mabao 2-0 yaliyofungwa na Enock Inonga na Kibu Denis.

Alisema kutokana na ubora wa Aishi Manula na Beno Kakolanya ulimpa matumaini ya kufanya vizuri na kuamini mchezo huo ni kama mingine.

“Kaka yangu Aishi alinitumia ujumbe muda mchache kabla ya mchezo na kuniambia kuwa nicheze kawaida kama ninavyocheza nikiwa katika mazoezi kwani hiyo ni mechi tu kama nyingine nilikuwa najiandaa mapema huku nikijua wao wanaocheza ni binadamu ipo siku wataumia”,alisema Salim ambaye alionyesha kiwango kizuri.

Salim alicheza mechi yake ya kwanza ligi kuu msimu huu dhidi ya Ihefu na alionesha kiwango bora akiokoa hatari zaidi ya mbili na kuwaacha wadau na mashabiki wengi wakishangaa uwezo wake.

Katika mchezo wa juzi dhidi ya Yanga alianza huku Simba ikiwakosa makipa wake namba moja, Aishi Manula na mwenzake, Beno Kakolanya haikuonekana pengo lao kutokana na kazi aliyoifanya Salim na kushinda 2-0.

Salim ambaye alipandishwa kutoka kikosi cha pili cha Simba 2017/18, anashindwa kujipenyeza katikati ya makipa hao wawili wanaochuana kuwania namba kikosi cha kwanza.

SOMA NA HII  KWA HALI HII YA SIMBA ROBERTINHO HANA MUDA MREFU