Home Habari za michezo KUELEKEA MECHI YA SIMBA NA YANGA…HAWA HAPA MAREFA WA MCHEZO HUO

KUELEKEA MECHI YA SIMBA NA YANGA…HAWA HAPA MAREFA WA MCHEZO HUO

KUELEKEA MECHI YA SIMBA NA YANGA...HAWA HAPA MAREFA WA MCHEZO HUO

WAKATI homa ya pambano la watani wa jadi ikianza kupanda kabla ya timu hizo kuvaana Jumapili ya wiki hii, SOKA LA BONGO limenasa faili ya waamuzi watakaopewa pambano hilo la 110 katika Ligi ya Bara tangu ilipoasisiwa mwaka 1965.

Simba na Yanga zitavaana kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam, huku Mnyama akiwa mwenyeji, akiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya 1-1 katika pambano la duru la kwanza lililopigwa Oktoba 23 mwaka jana.

Imezoeleka mara nyingi majina ya waamuzi wanaopewa pambano hilo hufichwa na kuja kutajwa siku moja kabla hazijashuka uwanjani, lakini safari hii SOKA LA BONGO limeweza kuyanyaka mapema majina ya waamuzi wanne watakaochezesha dabi hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi, Nassor Hamduni aliliambia SOKA LA BONGO  kuwa tayari majina manne kwa ajili ya pambano hilo yameorodheshwa, ila yatatangazwa muda muafaka ukishafika.

Mwamuzi huyo wa zamani wa kimataifa, alisema wameteua waamuzi wanne pekee na sio sita kama ambavyo huko nyuma ilivyokuwa ikifanyika katika dabi zilizokuwa na presha kubwa.

“Tumechagua majina manne ya waamuzi wenye uwezo mkubwa ambao wote wana kitambaa cha Fifa kutokana na kuwepo kwa mwenendo mzuri waliokuwa nao hivi karibuni kwenye ligi.

“Kwa sasa tunangoja kuyaidhinisha na Jumatano yatawekwa wazi ili kila mmoja ajue na tumefanya hivyo kutokana nani viwango vya waamuzi kuongezeka kwa sasa,” alisema Hamduni.

Kutokana na kauli ya bosi huyo huku ikifahamika Tanzania ina waamuzi wenye kitambaa cha Fifa kuwa ni 14 na mmoja wapo (Salum Siyah) anachezesha Ligi Kuu ya Zanzibar. Waamuzi 13 waliosalia wapo Ligi Kuu Bara ambapo watano wanachezesha katikati ambao ni Ahmed Arajiga, Ramadhan Kayoko, Tatu Malogona, Jonesia Rukyaa na Hery Sasii.

Kati ya waamuzi hao watano tayari waamuzi wawili walisimamishwa muda mrefu ambao ni Arajiga na Sasii, hivyo waamuzi watatu waliosalia Tatu Malogo pekee hajawahi kuchezesha dabi. Kutokana na kauli ya Hamduni bila shaka mwamuzi wa kati anaweza kusimama Kayoko au Rukyaa ndio wameonekana kwa siku za hivi karibuni wakitamba.

Kayoko ndiye mwamuzi aliyechezesha dabi iliyopita Oktoba 23 na endapo atasimama kati itakuwa rekodi kwake, kwani katika dabi 15 za mwisho hakuna mwamuzi aliyechesha dabi mfululizo.

Rukyaa mara ya mwisho kuchezesha dabi ilikuwa Januari 4, 2020 wakati timu hizo zikitoka sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa Ligi Kuu na safari hii anaonekana kuwa nafasi ya kupewa pambano hilo kutokana na mfululizo wa kupewa mechi zenye presha kubwa kwa hivi karibuni tangu arejee kazini.

Katika dabi 15, Sasii ndiye mwamuzi aliyehusika mara nyingi (13) akisimama katikati mara mbili na mwamuzi wa akiba akiwa mara 11 wakati,

Kayoko akiwa katikati mara nne, akisimama kama mwamuzi wa akiba mara mbili na pembeni mara mbili kwenye michezo waliokuwa waamuzi sita. Waamuzi wanaochezesha pembeni wenye beji ya Fifa wapo tisa ambao ni Hamdani Ally, Janet Balama, Yusuf Hashim, Tesha John, Frank Komba, Soud Lila, Mohamed Mkono, Kassim Mpanga na Rajab Ramadhan.

Pia Hamdun amethibitisha, Arajiga ni miongoni mwa waamuzi watakaopuliza kipyenga cha Afcon U17 mwaka huu baada ya kufanya vyema michuano ya Cecafa U17 mwaka jana na ile michezo ya kufuzu Afcon U17.

SOMA NA HII  KIFUNGO CHA MANARA CHAFUNGUA MIDOMO YA WADAU WA SOKA...WAIBUKA NA HOJA HIZI NZITO ZA KUSHINDILIA...

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here