news

SIMBA DAY KUPIGWA AGOSTI 6, AHMED ALLY ATAMBA

Staff Desk July 15, 2023 2:49 pm

TAMASHA la ‘Simba Day’ mwaka huu litafanyika rasmi Agosti 6 badala ya Agosti 8 kama ambavyo imezoeleka kila msimu kwenye timu ya Simba.

Tamasha hilo ambalo limekuwa kubwa na maarufu nchini limepangwa kufanyika Agosti 6 kutokana na ratiba kubana ndani ya kikosi hicho.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally amesema sababu ya kurudisha nyuma tamasha hilo ni kutokana na ugumu wa ratiba.

“Agosti 10 tutakuwa na mchezo wa nusu fainali ya Ngao ya Jamii dhidi ya Singida Fontain Gate kule Tanga hivyo tumeona ni vyema kurudisha nyuma siku mbili ili tuwape wachezaji mapumziko, naamini tunaweza kufanya vizuri katika hiyo mechi.”

Tamasha hilo litakuwa ni la 15 tangu lilipoanzishwa mwaka 2009 na aliyekuwa Mwenyekiti wa klabu hiyo, Hassan Dalali na katibu wake, Mwina Kaduguda.

SABABU ZA MAYELE KUITIKISA YANGA ZAWEKWA WAZI MZIZE ATAJWA ISHU YA CHAMA KWENDA YANGA IMEBAKI STORI, SIMBA WAZIMA NGOMA KIBABE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply