Home Tetesi za usajili YANGA SASA NI CHUMA BAADA YA CHUMA, WAMTAMBULISHA MCHEZAJI WAO MPYA SIO...

YANGA SASA NI CHUMA BAADA YA CHUMA, WAMTAMBULISHA MCHEZAJI WAO MPYA SIO POA

Baada ya kumtambulisha Winga Nickson Kibabage, Mlinzi Gift Fred kutoka Uganda, Kiungo Jonas Gerald Mkude alieachana na watani zao Simba SC.

Klabu ya Yanga imeendelea kuboresha kikosi chake baada ya leo kumtambulisha winga Maxi Mpia Nzengeli ukiwa ni usajili wao wa nne katika Dirisha hili kubwa la Uhamisho.

Nzengeli aliekuwa anachezea AS maniema amesaini Mkataba wa Miaka miwili na Yanga. Ujio wa Nzengeli ni kama Yanga wamekuja kuziba nafasi za mawinga wao Bernard Morisson na Tuisila Kisinda walioachana nao mwishoni mwa msimu uliopita.

Kwa ufupi huyu ndio Nzengeli,

Umri: 23

Urefu: Ft 5.7

Taifa: DR Congo

Ametoka: FC Maniema Union

Nafasi: Winga wa kulia / kushoto

Je, Mwananchi unauzungumziaje usajili wa Maxi Nzengeli? tupe Comment yako

SOMA NA HII  YANGA AKILI YOTE KWA SIMBA, LIGI KUU SASA NI VISASI TUPU