Habari za Simba leo
Habari za michezo

KUHUSU SIMBA KUTUMIA BILIONI 3 KWA KIPA MPYA….?, UKWELI WOTE HUU HAPA…

admin August 13, 2023 4:29 pm

KLABU ya Simba, imefanikiwa kumsajili kipa raia wa Morocco, Ayoub Lakred, akitokea FAR Rabat ambapo anaenda kuungana na Ally Salim, Hussein Abel na Aishi Manula ambaye kwa sasa ni majeruhi.

Kwa mujibu wa Mtandao wa Transfermarkt unaojihusisha na masuala ya takwimu na uhamisho wa wachezaji, thamani ya kipa huyo kwa sasa ni euro 1,200,000, sawa na Shilingi 3,281,436,000 (bilioni 3.3) za Kitanzania, hivyo Simba imefanikiwa kutoa kitita hicho kukamilisha usajili wake.

Kipa huyo amesaini mkataba wa miaka miwili kuanzia Agosti 11, 2023 na unatarajiwa kufikia tamati Juni 30, 2025.

Hivi karibuni Rais wa Heshima wa Simba, Mohamed Dewji ‘Mo’, alisema: “Nimetoa karibia bilioni 3 kufanikisha huu usajili, isitokee kwamba mtu aseme ‘Mo hajatoa hela’ tuepuke na wapotoshaji.”

Mo aliongeza kwamba: “Ali (Ally Salim) ni mzuri na Aishi ni Tanzania 1, hata hivyo ikiwa tunataka kushindana kwenye Ligi ya Mabingwa, Simba inahitaji kipa mwingine bora.”

Ujio wa Lakred ndani ya Simba, ni baada ya klabu hiyo kuachana na Mbrazili, Jefferson Luis ambaye siku chache tangu kusajiliwa kwake, alipata majeraha wakati timu ikiwa kambini Uturuki.

KWA RATIBA HII SASA YANGA WASHINDWE WENYEWE DAUDA AICHAMBUA YANGA YA GAMONDI, ASEMA HAYA KUHUSU DABI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply