Habari za Simba leo
Habari za michezo

AHMED ALLY AMTABIRIA BALEKE MVUA YA MAGOLI

Staff Desk August 25, 2023 11:29 am

Akiwa tayari ashapachika wavuni mabao 2 katika michezo miwili ya Ligi aliyocheza Mshambuliaji wa Simba SC, Jean Baleke.

Tayari wanasimba wameshamuwekea matumaini makubwa wakijinasibu kuwa moto alioanza nao hauwezi kuzikmika kirahisi.

Miongozi mwao ni Ofisa Habari wa Klabu ya Simba SC, Ahmed Ally ambae amesema kuwa msimu huu Straika huyo atafunga mabao 30.

Akizungumza Ahmed anasema;

“ Ninamtabiria makubwa mshambuliaji wetu Baleke msimu huu,ninaamini atafunga mabao kuanzia 30, hiyo ni kutokana na mwanzo mzuri alioanza nao, ”

“ Sio kitu kidogo kwake kufunga mabao mawili ndani ya michezo miwili, akiendelea kufanyia kazi maelekezo na mafunzo mazoezini, basi atafunga katika kila mchezo wa ligi, Kikubwa anachotakiwa kukifanya kuendelea na hapo alipoanzia, asibweteke na idadi ya mabao atakayoyafunga, ”

Je, unadhani Baleke atafunga mabao mangapi msimu huu?

BALEKE, PHIRI WATEGWA SIMBA SC, NGOMA AFUNGUKA ALICHOKIONA, KOCHA ATOA MSIMAMO HUKO SIMBA KIMEUMANA MWAMBA AGOMA KUTOLEWA KWA MKOPO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply