Afisa Habari wa Yanga SC Ally Kamwe
Habari za michezo

AZAM COMPLEX KUANZIA SASA IITWE YANGA COMPLEX ALLY KAMWE AFUNGUA HAYA

Staff Desk August 26, 2023 12:11 pm

Ofisa Habari wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe amewatupia dongo Klabu ya Azam baada ya kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na Klabu ya Bahri ya nchini Ethiopia jana usiku kwa mikwaju ya penati.

Kamwe amedai kuwa kwa vile Uwanja wa Azam Complex unatumiwa na Yanga, basi ubadilishwe jina na kuitwa Yanga Complex Chamazi mpaka pale ambapo Yanga italerejea kutumia dimba la Mkapa ambalo linakarabitwa.

“Tunatuma maombi kwa TFF na Bodi ya Ligi ule uwanja ubadilishwe kuanzia sasa uitwe Yanga Complex. Tunakwenda kimataifa, tukiulizwa na CAF, Yanga ni timu, je, hii Azam ni nini? Tutajibu nini? Ni kiwanda au nini? Kwa hiyo tutaita Yanga Complex mpaka tutakapoondoka pale.

“Azam hakuna timu pale, kesho (leo) tukutane Yanga Complex Chamazi, anayebisha alete timu pale. Kesho (leo) tunakwenda kutambulisha Maxi Day pale na kuutambulisha rasmi ule kuwa uwanja wetu,” amesema Kamwe.

MSEMAJI WA YANGA AWAAMBIA HAYA AL MARREIKH KIMATAIFA SKUDU ATOA KAULI NZITO BAADA YA KUREJEA NCHINI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply