Home news DIAMOND NAE AFUNGUKA HAYA BAADA YA YANGA KUPORWA NGAO YA JAMII

DIAMOND NAE AFUNGUKA HAYA BAADA YA YANGA KUPORWA NGAO YA JAMII

Habari za Yanga

Supastaa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amesema kuwa hana mpango wa kuihama klabu yake ya Yanga licha ya kupoteza mchezo wa Ngao ya jamii dhidi ya watani wao wa jadi, Simba Sc, juzi.

Mchezo huo ulipigwa katika Dimba la CCM Mkwakwani na Simba kufanikiwa kuibuka na ushindi kwa mikwaju ya penati 3-1 baada ya kutoa sare kwenye dakika 90 za mchezo.

Ikumbukwe Diamond aliwahi kuwa shabiki wa Simba kabla ya kuhamia Yanga wakati hasimu wake, Alikiba alikuwa Yanga na sasa amehamia Simba.

Chibu akiwa njiani kurudi Tanzania baada ya kumalisha show yake nchini Rwanda amesema; “Yanga sihami, kipofu kaona mwezi.”

Una maoni gani?

SOMA NA HII  ILE ISHU YA YANGA KUMSAJILI ULIMWENGU...UKWELI UKO HIVI....BOSI AANIKA MCHORO WOTE...