Home Habari za michezo ALLY KAMWE: YANGA HATUJAINGIA MAKUNDI YA CAF KWA MIAKA 20 ….

ALLY KAMWE: YANGA HATUJAINGIA MAKUNDI YA CAF KWA MIAKA 20 ….

Habari za Yanga

Klabu ya Yanga SC imekiri kwamba ina historia mbaya kwenye michuano ya Kimataifa kwani ina zaidi ya miaka 20 haijawahi kufika hatua ya Makundi ya Klabu Bingwa.

Kauli hiyo ameitoa leo Agosti 15, 2023 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo wao wa kwanza wa Klabu Bingwa dhidi ya Asasi utakaopigwa Jumapili hii katika dimba la Azam Complex-Chamaji jijini Dar.

“Tuna historia mbaya na michunao ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika, zaidi ya miaka ishirini timu yetu haijacheza hatua ya makunda, hatuwezi kuendelea kuiacha hii istoria iendelee miaka na miaka, tukubaliane kuwa mwaka huu ni wa mwisho.

“Msimu huu tuhakikishe timu yetu inakwenda kucheza hatua ya Makundi,” alisema Ally Kamwe.

SOMA NA HII  MANARA ALIPOGEUZA SIKU YA WANANCHI JANA KUWA FURSA KWAKE...AJIPA 'UMC' WA MITAANI...KITENGE AKAZIA YA TFF...